Quantcast
Channel: MRISHO'S BLOG
Viewing all 4405 articles
Browse latest View live

Mazungumzo na mtangazaji Rose Chitallah kwenye kipindi cha JUKWAA LANGU

$
0
0
Mubelwa Bandio na Rose Chitallah studioni
Kipindi hiki ambacho kinakujia kila JUMATATU, kinajadili mambo mbalimbali na zaidi kuhusu UCHAGUZI MKUU WA TANZANIA 2015
Katika kipindi hiki utasikia mahojiano yetu na watu mbalimbali kuhusu DEMOKRASIA kuelekea uchaguzi nchini Tanzania
Katika kipindi cha wiki hii tumebahatika kuungana na mtangazaji Rose Chitallah
Karibu

MMLIKI WA ST. MATHEW, ST. MARK ADAIWA TALAKA NA MGAWANYO WA MALI

$
0
0
court_gavel
Na Mwandishi Wetu
MDAI katika kesi ya madai ya talaka na mgawanyo wa mali Magreth Mwangu mkazi wa Mkoani Singida dhidi ya Mkurugenzi wa Shule za sekondari za St.Mathew na St Marks Thadei Mtembei amelalamikia kitendo cha Benki ya CRDB kutoa taarifa zake za benki bila idhini yake wala ya mahakama.

Pia ameilalamikia mahakama ya Mwanzo Kizuiani inayosikiliza kesi hiyo kwa kutumia Wakili wa kujitegemea licha ya kuwa mawakili hawaruhusiwi katika mahakama ya Mwanzo.
Kesi hiyo inasikilizwa na hakimu Rajab Tamaambele.
Wakili huyo amekuwa akimwakilisha mdaiwa ambaye amekuwa hafiki mahakamani tangu kesi hiyo ifunguliwe kwa kile kilichoelezwa wamepata kibali kutoka kwa mwanasheria mkuu wa serikali kinachoruhusu kesi hiyo kusikilizwa na wakili bila mdaiwa kuwepo.
Kwa mujibu wa Mwangu tangu kesi hiyo ianze kusikilizwa mahakamani hapo mdaiwa amekuwa hafiki mahakamani na badala yake amekuwa akiwakilishwa na mtoto wake,Peter Mtembei ambaye ni Wakili hali iliyofanya kesi hiyo mpaka inaisha na kufungwa ushahidi mdaiwa akiwa hajasikiliza shahidi hata mmoja.
Hata hivyo Mmiliki huyo wa St, Mathew juzi alifika mahakamani kufuatia amri ya mahakama kufuatia malalamiko ya mdai aliyokuwa akitoa mahakamani kutokana na Mtembei kushindwa kufika kwenye kesi hiyo tangu ilipofunguliwa na iliyomtaka afike mwenyewe mahakamani hapo na endapo asingefika mahakama ingehamia nyumbani kwake.
Akitoa ushahidi wake, Mtembei alisema alifahamiana na Mwangu wakati akiwa na mfanya usafi katika duka lake la dawa.
Alisema hakuwahi kumuoa mama huyo wala kuishi naye licha ya kuzaa naye watoto watatu.
Alisema mama huyo hana hadhi ya kuwa mke wake kwani ameishia darasa la saba elimu ambayo ni ya chini sana.
“Huyu alikuwa ni mfanya usafi tu ni nesi msaidizi kazi yake ilikuwa ni kufanya usafi na hata kufunga vidonda tu” alisema.
Alisema duka hilo la dawa lilifungwa baada ya kuonekana aliyekuwa analihudumia hana elimu.
Mtembei alisema mdai hana uhusiano na mali alizonazo kwani yeye ana mke wake wa ndoa na huyo alikuwa ni mwanamke tu aliyezaa naye.
“Huyu ni mwanamke tu niliyezaa naye hana haki kwenye mali zangu” alisema
Alipohojiwa na mahakama kama alifunga ndoa na mdai alisema kuwa hajawahi kufunga naye ndoa licha ya kutoa mahari ya Ng’ombe watano. “Nilimpelekea baba yake vindama vitano tu kama zawadi” alisema
Alisema hajawahi kufunga ndoa ya kimila na mdai kama inavyodaiwa na mdai hana haki yoyote katika mali zake.
Kwa upande mwingine mdai alihoji sababu za mdaiwa kwenda Benki ya CRDB na kutoa taarifa za fedha za akaunti yake bila kuwa na amri iliyotolewa na mahakama.
“Mdai kwa kutumia nafasi nzuri ya kifedha aliyokuwa nayo ameweza kwenda benki ya CRDB na kupewa taarifa za fedha kwenye akaunti yangu bila ruhusa yangu au ruhusa ya mahakama jambo ambalo limeniathiri kisaikolojia’ alisema
Hata hivyo hakimuTamaambele alisema hafahamu ni wapi mdaiwa alitoa taarifa hiyo lakini mahakama inaipokea kuwa sehemu ya ushahidi.
Kesi hiyo imepangwa kutolewa hukumu Agosti 25, mwaka huu.
Katika kesi hiyo mdai anaiomba mahakama imuamuru mdaiwa kupa takala,kutoa Sh. Milioni 800 na makazi ya kukaa mdai na watoto wake.

SAVING FOR A BETTER FUTURE

$
0
0

By Krantz Mwantepele 

Financial planning is an essential tool for anyone to get what they want out of life. This tool helps with things such as living within your income, identifying financial priorities, meeting financial emergencies and saving and investing to reach financial goals. All this can be done if you know the value of money in relation to your plans and achievements in life.

Saving money means finding smart ways to maintain your standard of living while putting money aside at the same time. You have to know some of the common myths regarding saving money and then take action. You can save money starting today, and you can do it in any way that makes sense for you and your lifestyle.

Don't believe all the bad information and myths regarding saving money, and don’t let false information keep you from achieving your financial goals. One of the common myths about saving money is that it takes too long to save.

For example, if you punish yourself by lowering your standard of living every time you want to save money, you'll hardly feel motivated to save. Instead, get creative. Brainstorm ways to make more money on the side, preferably by setting up passive streams of income.

The African financial services industry is rapidly evolving as a result of advancing technology, which fuels innovation and growth in the sector. In most developed countries, the sector is mature, but it’s less saturated in Africa. Due to this, there are many opportunities for new market entrants to challenge the status quo of how business has traditionally been conducted.

In Africa, there have been great innovations in the area of mobile banking and e-commerce businesses, which has led to a shift in the banking institution. In sub-Saharan Africa, where less than 24 percent of the population has a bank account and over 60 percent have a mobile phone, most telecommunication companies offer easy-to-use mobile financial services that allow transactions to be made remotely and securely, avoiding the need to carry money around.

Now, customers can transfer money from their mobile phones to any other customer in the country and, in some countries, internationally. They can also pay their water, electricity and television bills and top up their airtime remotely. Depending on the country, they may also benefit from a savings and insurance solution.

For me, saving was a great challenge because of the innovation of mobile money – all my transactions were done using mobile money and I was just interested in taking care of basic needs. But savings, especially when using a bank, can be good for meeting specific goals.

I’ve learnt that, beyond savings, investing can help me achieve bigger financial goals such as a dream home or an early retirement. That's because money is invested in assets such as bonds, shares, alternatives, property and even currency, which has the potential to grow much faster than the rate of inflation or money on deposit. Just like saving, I can invest small or big amounts and on a one-off lump sum or regular basis.


This article is the first in a series of sponsored posts for the Barclays Savings Challenge. Follow the discussion on Twitter and Face book and share your own experience by using #AfricaSaves.

SIMU MPYA WA KANDANDA NDANI YA DSTV KUTIMUA VUMBI WIKI IJAYO

$
0
0
IMG_0388
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho wa msimu mpya wa kandanda kwa wateja wa DStv jana jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu na kulia ni Meneja Mwendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog).
IMG_0397
Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo, akijibu maswali ya waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na huduma za DStv. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi.

IMG_0422
Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu, akielezea huduma za kuunganishwa kwa wateja wapya wa DStv, ambapo ving'amuzi pamoja na dishi vinapatikana kwa gharama nafuu kabisa ya Sh.99,000/- kwa mawakala wote wa DStv nchini.
IMG_0443
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi (wa pili kushoto) akikabidhi zawadi ya begi kwa mwandishi wa habari, Joseph Michael baada ya kuchezesha droo kwa waandishi waliohudhuria mkutano huo. Wanaoshuhudia kushoto ni Afisa Masoko wa Multichoice Tanzania, Furaha Samalu na kulia ni Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.
IMG_0454
Furaha Samalu na Barbara Kambogi wakikabidhi zawadi ya begi Super Sport kwa mpiga picha wa ITV, Abdallah Kaniki aliyeibuka mshindi katika droo iliyochezeshwa na Multichoice Tanzania wakati wa mkutano na waandishi wa habari. Kulia Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Baraka Shelukindo.
IMG_0458
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi akikabidhi zawadi ya T-shirts kwa mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Imani Makongoro.
IMG_0419
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Na Andrew Chale, modewjiblog
Msimu mpya wa Soka 2015/16, unatarajia kuanza rasmi Jumapili ijayo kwa kushuhudia ligi mbalimbali Duniani zikichezwa na kurushwa moja kwa moja kupitia SuperSport ambayo imejipanga kukuletea burudani kabambe kwa mashabiki wa soka barani Afrika.
Meneja uendeshaji wa Multichoice Tanzania , Ronald Baraka Shelukindo mapema jana akizungumza na vyombo vya habari amebainisha kuwa, Wateja wa DStv wakae tayari msimu huu kwenye Ulimwengu wa Mabingwa ambapo timu mbalimbali zimejiimalisha katika kuakikisha zinatwaa ubingwa.
“Ligi ya mwaka zitakuwa za kasi na kuvutia kwa kila timu. Barcelona wanajiandaa kutawala dunia kwa mara nyingine, huku Manchester United wanahitaji kurudisha kiti chao cha Ubingwa Uingereza. Jose Mourinho analenga kuhakikisha Chelsea inabaki juu, wakati huo huo , Hispania inajiandaa kuhakikisha wanashinda kwa mara ya tatu kombe la Euro 2016.” Ameeleza Baraka Shelukindo.
Ameogeza kuwa, Watazamaji wa SuperSport watakuwa na nafasi ya kipekee kushuhudia mechi kwenye ubora wa HD, ikiwa ni pamoja na michuano ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) , Ligi ya Hispania (La Liga) , Ligi ya Mabingwa wa Ulaya(UEFA) na Ligi ndogo ya Ulaya ( Europa) ,mechi za FIFA za kirafiki za kimataifa na Klabu Bingwa ya Dunia , Kombe la Ujerumani , Kombe la Mfalme Hispania (Copa Del Rey) , Kombe la FA na zaidi.
Kwa upande wake, Meneja Uhusiano wa Multichoice Tanzania, Barbara Kambogi anaeleza kuwa, Katika msimu huu , Ulimwengu wa Mabingwa itakuwa ikionyesha mechi zaidi ya 900 za kimataifa. Wateja wa DStv Compact Plus wataweza kufurahia baadhi ya mechi zaidi ya 450 ‘live’, huku Wateja wa DStv Premium watazawadiwa mechi zote ‘Live’ zitakazorushwa katika chaneli zote za SuperSport .
“Kuanzia msimu huu na kuendelea, vituko vyote vya Ligi Kuu ya Uingereza vitakuwa vikiletwa kwenu kupitia SuperSport 5 ( SS5 ) inayopatikana kwenye kifurushi cha Premium. SS5 sasa itakuwa ni nyumba ya soka la Afrika kwa ligi kuu ya Uingereza huku ikijumuisha mechi 3 ‘Live’ kila Jumamosi na Jumapili. Kuambatana na mechi kutakuwa na vipindi maalum vya soka kama PLTV Kick Off, Match Day Live, Fan Zone, Saturday/Sunday Review, Football Today, Classic Matches, Netbusters na Mech za Wiki” Amebainisha Barbara Kambogi.
Moto wa La Liga utawashwa ndani ya SuperSport 3 ( SS3 ). Chaneli hii itakuwa inakuletea mechi hadi tatu za ligi ya Hispania ‘ Live’ kwa siku ya Jumamosi na Jumapili . Wateja wa DStv Premium na Compact Plus watapata nafasi ya kuangalia mechi za michuano ya Kombe la mashindano Uingereza ndani ya SS3 sambamba na mechi za Jumamosi mchana za Ligi kuu ya Uingereza , mbadala wa mechi inayorushwa ndani ya SS5, pamoja na Ratiba zote za Jumatatu usiku na vipindi vya mahojiano vya studio.
Pamoja na Mechi za ‘Live’ ndani ya SS3 , itakuwa inakuonyesha vipindi muhimu vya shoo za magazeti , yanayojiri ndani ya La Liga, pamoja na vipindi maalum vya ligi za soka . Makombe yote ya mpira wa miguu, Mabingwa wa Ulaya na Ligi ya Europa, Kombe la FA , Kombe la Mfalme Hispania (Copa Del Rey), Kombe la Ujerumani , Euro 2016 na mechi za kirafiki za kimataifa zitaendelea kutapatikana kwenye SS3 .
Kwa habari zaidi za michezo na ratiba za mechi kwenye SS5 na SS3, tafadhali tembelea www.supersport.com

GARI LA KUBEBEA MAJENEZA LA KIPEKEE LAINGIA NCHINI

$
0
0
IMG_0469
Pichani juu na chini ni muonekano wa Gari maalum la kukodisha kwa ajili ya shughuli za kubebea majeneza katika misiba limeingia nchini.
Kwa wanaohitaji kukodi kwa shughuli za misiba wanaweza kuwasiliana kupitia barua pepe kiwiaadavidson@hotmail.com au simu namba +255 715 213213, +255 713 616606 na +255 784616606
IMG_0459
IMG_0481
Muonekano wa ndani sehemu maalum linapowekwa jeneza.
IMG_0477

Simba Imeshinda katika mchezo wake wa Pili wa Mazoezi

$
0
0
Kikosi cha Timu ya Black Sailor iliopanda daraja mwaka huu kucheza Ligi Kuu ya Zanzibar kwa Msimu wa mwakac 2015/2016, ilikubali kupigo cha mabao 4--0 dhidi ya timu ya Simba katika mchezo wa kirafiki uliofanyika usiku huu katika uwanja wa amaan Zanzibar. 
Kikosi cha Simba kilichotoa kipigo kwa Timu ya Black Sailor uwanja wa Amani usiku huu Simba ikiwa Zanzibar kwa michezo ya kirafiki kuimarisha Kikosi chake kujiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania.
       Jopo la Makocha wa timu ya Simba wakifuatilia mchezo huo wa kirafiki na timu ya Black Sailor
Mchezaji wa timu ya Simba akikokota mpira akijiandaa kumpita beki wa timu ya Black Sailor, wakati wa mchezo wao wa kirafiki uliofanyika uwanja wa amaan timu ya Simba imeshinda 4--0
Mchezaji wa timu ya Black Sailor akiwapita wachezaji wa timu ya Simba katika mchezo wa kirafiki.
                    Mshambuliaji wa timu ya Simba akimpita beki wa timu ya Black Sailor

Mchezaji wa timu ya Simba Abdi Banda akiifungia timu yake bao la kwanza kwa kichwa katika mchezo huo wa kirafiki uliofanyika uwanja wa Amaan timu ya Simba imeshinda bao 4--0
Wachezaji wa Simba wakishangilia bao lao la kwanza lililofungwa na mchezaji Abdi Banda kwa kichwa baada ya kupigwa krosi na Khamis Kiiza, mwenye jezi namba 5
Mshambuliaji wa timu ya Simba akimpita beki wa timu ya Black Sailor wakati wa mchezo wao wa kirafiki.
              Mshambuliaji wa timu ya Simba Khamis Kiiza akimpita beki wa timu ya Black Sailor


Mshambuliaji wa timu ya Simba na Black Sailor wakiwania mpira wakati wa mchezo wao wa kirafiki uliofanyika uwanja wa Amaan Zanzibar timu ya Simba imeshinda 4--0 mchezo uliofanyika usiku huu.
Mshambuliaji wa timu ya Simba akizuiya mpira huku mabeki wa timu ya Black Sailor wakijiandaa kumzuiya.
       Kipa wa timu ya Black Sailor akidaga mpira ikiwa moja ya ulio gplini kwa timu ya Black Sailor
Mshambuliaji wa timu ya Simba akiruka kiunzi cha beki wa timu ya Black Sailor wakati wa mchezo wao wa kirafiki uliofanyika uwanja wa Amaan Timu ya Simba imeshinda 4--0
Goli la pili la timu ya Simba lililofungwa na mshambuliaji Ibrahim Hashim katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo wa kirafiki uliofanyika uwanja wa amaan timu ya Simba imeshunda 4--0
                           Beki wa Timu ya Black Sailor akiokoa mpira galini kwake
Mchezaji wa Simba akiwa juu akipiga kichwa golini kwa timu ya Black Sailor.
Beki wa timu ya Black Sailor akioko mpira golini kwake wakati wa mchezo wa kirafiki uliofanyika katika uwanja wa Amaan Timu ya Simba imeshinda 4--0.
Picha na OthmanMapara.Blog. Zanzinews.com  

Angalia Kipindi Chote Cha 'Nyumbani Na Diaspora' TBC1 Jana Ijumaa.

$
0
0
Nyumbani na Diaspora!
Ni kipindi kipya cha saa nzima chenye kuhusiana na Watanzania wa nyumbani na walio nje ya mipaka yetu. Ni kipindi daraja kitakachowaunganisha Watanzania katika kubaini fursa mbalimbali za kuinuka kimaendeleo, kwa mtu mmoja mmoja, jumuiya na hatimaye taifa. Ni kipindi kitakachoongozwa na mchambuzi na mmoja wa wanahabari nguli hapa nchini. Si mwingine ni Maggid Mjengwa. Jiunge nae kufuatilia mahojiano motomoto na watu wa kada tofauti kwenye masuala ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kitamaduni. Ni kila siku ya Ijumaa saa 4 usiku na marudio Jumapili saa kumi jioni, TBC 1, ukweli na uhakika!

UCHAMBUZI WA MAGAZETI ASUBUHI YA LEO AGOST 2

$
0
0
Je unafahamu nini kimeandikwa juu ya kura za maoni ndani ya CCM magazetini leo baada ya Mchakato wa uchaguzi hapo jana?Tazama uchambuzi.

Je wafahamu dondoo za uchaguzi ndani ya CCM baada ya kura za maoni kufanyika hapo jana? Tazama hapa uhabarike.

Je wafamu ni habari gani za michezo zimepewa kipaumbele katika magazeti ya leo? Furahia uchambuzi hapa.

WATANZANIA CALIFORNIA WAMUAGA BALOZI LIBERATA MULAMULA

$
0
0
 Watanzania California wakiongozwa na Balozi wa Heshima Mhe. Ahmed Issa walijumuika pamoja siku ya Ijumaa na kumuaga Balozi Liberata Mulamula anayemaliza muda wake kama Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico na kurudi nyumbani kwenda kulitumikia taifa kama Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 Watanzania wa California wakipiga picha ya pamoja na Mhe. Balozi Libarata Mulamula (wapili toka kushoto) siku ya Ijumaa July 31, 2015 walipomuaga rasmi.
 Balozi Liberata Mulamula akimkabidhi zawadi yake Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme mara tu baada ya kukabidhiwa na Watanzania California siku ya Ijumaa July 31, 2015 walipomualika rasmi kwa ajili ya kumuaga.
 Balozi Liberata Mulamula akicheza na kuburudika kwenye moja ya nyimbo zilizopigwa kwenye tafrija hiyo.
 Balozi Liberata akipiga makofi
Moja wa kikundi maarufu cha ngomma ya asili kikitoa burudani

MAANDALIZI YA UFUNGUZI WA BIDHAA MPYA ZA OIL WAKAMILIKA

$
0
0
Aina mpya Oil ya magari na mitambo ya NEXTOIL imeingia nchini na kesho inazinduliwa rasmi chini ya duka la F-ZONE (T) LIMITED lililopo jijini Dar es salaam Mtaa wa Kariakoo na Msimbazi. Wasiliana nao kwa simu +255 757222480

Sehemu ya shehena ya NextOil kutoka Triton kama inavyoonekana kwenye duka la F-Zone (T) Limited lililopo mtaa wa Msimbazi Kariakoo, Dar.

MTOTO WA MAMA NTILIE JUMAA AWESO ASHINDA KWA KISHINDO UCHAGUZI WA NDANI CCM PANGANI

$
0
0
aweso
Ndugu Jumaa Aweso.
Na Mohammed Hammie, Pangani, Tanga
Mtoto wa mama ntilie mwenye uzao halisi kutoka wilayani Pangani mkoani Tanga, Ndugu Jumaa Aweso (pichani) ameibuka na ushindi wa kishindo katika uchaguzi wa ndani wa chama cha mapinduzi CCM.

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo katibu wa CCM wilayani Pangani Bi Zaina Mlawa amesema kuwa, katika uchaguzi huo uliowashirikisha wagombea wapatao kumi na moja, Ndugu Aweso amekuwa wa kwanza miongoni mwa wagombea hao.
Uchaguzi huo uliokuwa na ushindani wa aina yake kutokana na kuwepo kwa aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo Ndugu Salehe Pamba, uliwashirikisha wapiga kura wapatao 10376 wa chama cha mapunduzi.
Awali wakati akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Bi Zania aliwataja wagombea hao kwa idadi ya kura walizopata na kusema kuwa "Ndugu Wahi Ibrahim amepata kura 87, ndugu Rosemary Luanda amepata kura 89, ndugu Elizabeth Alatanga amepataa kura 158, Halima Kimbau amepata kura 222, Ndugu Mohammed Rished amepata kura 442, Ndugu Ayubu Mswahili amepata kura 565"
Bi Zania ameongeza kwa kusema kuwa "Ndugu Omary Mwidadi amepata kura 587, ndugu Omary Chambega amepata kura 720, ndugu Salehe Pamba amepata kura 1567, ndugu Abdurahmani magati amepata 1956, na ndugu Jumaa Aweso 3983"
Ushindi huo kwa ndugu Jumaa Aweso unampa nafasi ya kuwa mgombea wa kwanza katika kuipeperusha bendera ya chama cha mapinduzi CCM wilayani Pangani endapo kamati kuu ya maamuzi itaridhia.
Mpaka sasa katika jimbo la Pangani kumepatikana wagombea wawili ambao wanaonekana kupendwa sana na wanancho ambao ni Amina Mwidau wa CUF pamoja na JUmaa Aweso wa CCM ambapo kwa mujibu wa wachambuzi wa masuala ya siasa, endapo watakutana katika nafasi ya ubunge upinzani utakuwa wa aina yake.

KILA LA HERI BINTI YETU ZAHARA KWENYE KURA ZA MAONI ZA UBUNGE WA CCM VIJANA MKOANI TABORA

$
0
0

Na Jeff Msangi 
wa TBN Ughaibuni
Nyota njema huonekana asubuhi. Bila shaka umewahi kusikia msemo huu. Kwa Zahara Muhidini Issa Michuzi, nyota yake njema ni tunu ya uongozi. Tangu alipoweza kutambua maana na tofauti ya jambo jema na baya, amekuwa kiongozi.
Muhtasari wa maisha yake unaonyesha alizaliwa mnano tarehe 2 Septemba mwaka 1987 Nzega mkoani Tabora. Amesomea katika shule zifuatazo;
*Shule Ya Msingi Rufita, Tabora- 1995-2001
*Shule Ya Sekondari Kazima, Tabora-2002-2005
*Shule Ya Sekondari Ya Juu Emma, Kampala-Uganda 2007-2009
*Chuo Kikuu Cha Dodoma, Dodoma,Tanzania 2011-2014.

Zahara Muhidini Issa Michuzi, ambaye ni binti wa Ankal, ni mhitimu wa Shahada ya Sanaa katika masuala ya Uchumi. Mpaka kufikia hapa alipo, nyota yake ya uongozi imejidhihirisha katika sehemu mbalimbali alizopitia hususani shule.
Amekuwa kiranja, msimamizi  wa shughuli na miradi mbalimbali shuleni na alipokuwa Chuo Kikuu Dodoma alikuwa kiongozi katika Jumuiya ya Wanafunzi- University of  Dodoma Students Organization (UDOSO) akiwa kama Mbunge wa Baraza La Wanafunzi.
Mbali ya uzoefu wa kiuongozi alionao, Zahara anazo sifa zifuatazo ambazo ni nadra na tunu kubwa katika uongozi;
Anajitambua- Zahara anajitambua vilivyo. Anatambua kwamba uongozi ni heshima na utumishi uliotukuka.
Ana Ari Ya Kuongoza na 
Kujifunza- Zahara anaamini kwamba kiongozi bora lazima awe ana ari ya kuongoza na kutumikia wananchi anaowaongoza. Mbali ya kuongoza,kiongozi lazima awe tayari kujifunza kutokana na hali halisi na kukabiliana na mabadiliko ya aina yoyote yanayoweza kujitokeza.
Ni Msikivu Na Ana uwezo Mkubwa wa Kufanya Kazi na Watu- Hili Zahara amelithibitisha katika ngazi zote za kiuongozi ambazo amepitia. Usikivu wake umekuwa chachu ya kumwezesha kutatua matatizo mbalimbali ambayo amekabiliana nayo huku yeye kama kiongozi akitarajiwa kuyatatua.
Ana Uwezo Wa Kuongoza Mabadiliko Ya Kijamii- Zahara anaamini kwa vitendo kwamba jamii yoyote lazima isonge mbele ili kwenda sambamba na mabadiliko mbalimbali ya kijamii. Anaamini kwa vitendo kwamba uongozi thabiti unahitajika ili kuleta mabadiliko chanya ambayo jamii yoyote inahitaji. 
Zahara Muhidini Issa Michuzi hivi sasa anagombea kuwa mwakilishi wa vijana Bungeni kupitia Viti Maalumu Vijana (Youth Seats) kupitia Chama Cha Mapinduzi(CCM)- Tabora. Anaomba Kura na Ushirikiano Wako.

 Ankal akifurahi na binti yake Zahara siku ya Maulid maalumu ya kusherehekea kuhitimu digrii ya Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma mwaka jana. Hii ndiyo siku ambayo Zahara aliweka nia hadharani kwamba angependa kugombea Ubunge mkoani Dodoma ili kumuenzi marehemu mama yake kwa kuwatumikia wananchi wa mkoa huo kwa moyo wake wote.
Zahara akifurahi na Mama yake mlezi
 Zahara akiwa na dada zake
 Zahara akiwa na familia yake
 Zahara akiwa na baba yake mzazi, Ankal
 Zahara akiwa na baba yake na Mama yake Mlezi ambaye ni dada wa marehemu mama yake, Bi Rehema Saidi
Zahara akiwa na baba na wadogo zake.


       

MMLIKI WA ST. MATHEW AIHAMISHA MAHAKAMA KWA GHARAMA ZAKE

$
0
0
court_gavel
Na Mwandishi Wetu, Singida
MDAI katika Kesi ya madai ya talaka Magreth Mwangu dhidi ya Mkurugenzi wa Shule ya St. Mathew, Thadei Mtembei amehoji uhalali wa mahakama kufikia kukagua mali zake siku ya Jumamosi bila kupitia mahakama yoyote hapa Singida.

Kesi hiyo ambayo inasikilizwa mahakama ya Mwanzo Kizuiani Mbagala Jijini Dar es Salaam, juzi (Jumamosi) ililazimika kuhamia mkoani Singida baada ya mdaiwa (Thadei Mtembei) kuitaka mahakama kuhamia mkoani Singida kwa gharama zake ili kuhakiki nyumba ambazo alidai alimjengea Mwangu.
Mtembei katika hoja yake ya kuitaka mahakama kuhamia Singida alisema yuko tayari kulipa gharama zote ikiwemo nauli na posho.
Hakimu anayesikiliza kesi hiyo Rajab Tamaambele, na wakili wa Mtembei ambaye ni mtoto wa mke mkubwa wa Mtembei (Peter Mtembei), karani na kesi na mtumishi wa mahakama ni miongoni mwa watu waliofika kwa ajili ya ukaguzi na uhakiki wa nyumba hizo.
Hata hivyo hakukuwepo na wazee wa baraza jmbo ambalo mwangu pia alililalamikia. Mwangu alidai kuwa licha ya kuwa hafahamu sheria kutokana na kutokuwa na elimu hata ya Sekondari lakini kitendo cha mahakama kufika Jumamosi kwa ajili ya kufanya uhakiki na ukaguzi haioni kama ni ha haki na pia kulikuwa hakuna afisa ustawi wa jamii.
Alidai hakimu kuongozana na wakili wa kesi hiyo na kuwa pamoja muda wote haoni kama atatendewa haki katika shauri hilo.
“Mimi nahoji ushirikiano huu kama utanitendea haki kwani watu wametoka pamoja Dar es Salaam wameongozana kwenye magari binafsi nafika eneo la tukio nakuta msafara wa hakimu, wakili wa mdaiwa, mwenyekiti wa kitongoji ukiwa umeshafika mbele ya nyumba ambayo walitaka kuanza kuihakiki” alidai.
Alidai hata Mwenyekiti wa Mtaa wa Sabasaba, Mahamoud alisema hajapewa taarifa yoyote ya maandishi kwani alishtukizwa na kupelekwa kwenye nyumba hiyo ambayo alisema hafahamu kama ni ya Mwangu.
Pia alihoji uhalali wa mtoto wa Mtembei ambaye ni wakili kusimamia shauri hilo katika mahakama ya Mwanzo huku mara kadhaa akimtolea maneno ya kashfa kama ni mfunga vidonda tu hawezi kujenga nyumba.
Mwangu alisema alishawahi kuiambia mahakama kuwa nyumba zake za Singida alizijenga na aliamua kuziuza kwa ajili ya elimu ya watoto wake ambao walitelekezwa na baba yao lakini cha kushangaza mahakama kwa amri ya Mtembei ikataka kufika Singida kuhakiki nyumba zake.
Hata hivyo mahakama ilikagua nyumba tatu ambapo moja ilikuwa imeshauzwa kwa Sh. Milioni 15 na nyingine iliuzwa ikiwa katika hatua ya msingi.
Baada ya kumalizika kwa uhakiki huo hakimu Tamaambele alimtaka Mwangu kuhakikisha anawasilisha mahakamani nyaraka zote za nyumba na kuwapeleka watoto mahakamani kabla ya kesi hiyo kutolewa hukumu Agosti 25, mwaka huu.

FILAMU YA AISHA YAZINDULIWA KWA KISHINDO WILAYANI PANGANI

$
0
0
1- moja
Filamu iliyopewa jina la AISHA imezunduliwa rasmi siku ijumaa ya tarehe 31/7/2015 wilayani Pangani chini ya shirika lisilo la kiserikali la UZIKWASA.

Filamu ya aisha ni kwa heshima ya wanawake wote waliopitia mikasa ya namna hii.
8- nane
Mkuu wa wilaya ya Pangani Bi Regina Chonjo ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi, nae alipata nafasi ya kutoa hotuba yake.

6- sita
Producer wa filamu ya Aisha Bwana Emil Shivji akizungumza na wananchi waliohudhuria viwanja vya Bomani.
7- saba
Mkurugenzi wa shirika la UZIKWASA Dokta Vera Piroth akitoa hotuba yake ya kipeke ambayo ilikuwa katika mtindo wa hadithi pamoja na maswali, Ilipendeza sana.
2- mbili
Shamra shamra za ngongoti zikikaribisha wageni waalikwa kwenye uwanja wa Bomani wilayani Pangani palipofanyika uzinduzi wa flamu ya Aisha.
3- tatu
Msanii maafuru wa mashairi Ndugu Mabwingo akitoa burudani jukwaani.
4- nne
Wananchi wakiendelea kufatilia uzinduzi wa filamu ya Aisha.
5- tano
Msanii mahiri katika uimbaji, Vitalis Maembe alikuwepo kwenye uzinduzi wa filamu ya Aisha, alitoa burudani ya kipekee.
9- tisa
Wasanii waliocheza filamu ya Aisha wakiwa katika picha ya pamoja wakati wakipokea zawadi zao za ushiriki.
11- kumi na moja
Washereheshaji katika uzinduzi wa filamu ya Aisha, Mohammed Hammie maarufu kama Anko Mo (kati kati), Nickson Lutenda aliyevaa koti la bluu pamoja na Pili Mlindwa.
12- kumi na mbili
Mkurugenzi wa shirika la UZIKWASA akiteta jambo na mkuu wa wilaya ya Pangani Bi Regina Chonjo.
10- kumi
Msanii Godliver Gordian ambaye amecheza kama Aisha katika filamu hiyo, akifanya mahojino na kituo cha luninga cha TBC ambao walikuwepo katika uzinduzi huo.
13- kumi na tatu
Msanii Vitalis Maembe akiwa na Godliver Gordian (Aisha), wakati wa utambulisha wa wimbo uliotumika kama soundtrack katika filamu hiyo.
14- kumi na nne
Godliver Gordian ama Aisha akiwa na mshumaa mara baada ya wananchi kuitazama filamu ya AISHA- lengo la mshumaa huo ni kumulika unyanyapaa, pamoja na aibu wanayoipata wanawake na wasichana wanapotendewa matendo maovu.
15- kumi na tano
Wageni waalikuwa wakiongoza na mkuu wa wilaya Pangani Bi Regina Chonjo nao waliwasha mishumaa katika kumuunga mkono Aisha katika harakati za kufichua maovu.
16- kumi na sita
Wananchi wengine pia waliwasha mishumaa kuashiria kuunga mkono harakati hizo.
Aisha ni filamu ya tatu katika mfululizo wa filamu za UZIKWASA zikiangazia aina mbali mbali za unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto wa kike. Filamu hizi ni ni sehemu mojawapo tu ya njia za mawasiliano katika kampeni shirikishi-jamii ya mabadiliko ya tabia inayofahamika kama 'BANJA BASI'!, Pangani, Tanga.
Kabla ya filamu ya Aisha iliyozinduliwa kwa kishindo hivi karibuni, shirika la UZIKWASA tayari limeshatengeneza filamu nyenigne mbili ambazo ni FIMBO YA BABA na CHUKUA PIPI, wengi wa waigizaji waliomo ni wasanii wa vijijini.
Pia filamu hizi zinatokana na maisha halisi na utafiti wa kina katika jamii. Kwa nji hii UZIKWASA inahakikisha filamu zake zinaeleweka na zinafanya kazi kama kioo wka jamii. Lengo ni tuone, tuguswe na hatimaye tuchukue hatua ili kuleta mabadiliko.
Filamu ya AISHA inamhusu mwanamke anayeishi mjini na kuamua kurudi kijijini kwao kuhudhuria harusi ya mdogo wake. Wakati anajikumbusha maisha yake ya zamani, na kukutana na familia yake pamoja na marafiki, kunatokea mkasa wenye athari kubwa katika maisha yake.
Watu wangefumbia macho mkasa huo, lakini Aisha anaamua kupambana nao vikali ili kupata haki yake.
Filamu hii inahusu unyanyaa, aibu na wahanga kulaumiwa, na namna gani inazuia wanawake na wasichana kusema wazi. Pia inahusu baadhi ya mamlaka na viongozi kusita kufatilia ukiukaji wa haki za binadamu.
AISHA imeongozwa na mtaalamu maarufu Chande Omar, imetayarishwa kwa ushirikiano na Kijiweni Production, imefadhiliwa na A. Schindler na Swiss Development Cooperation (SDC) na kusimamiwa na shirika la UZIKWASA.

WAKRISTO WA ITALIA WAWEZESHA ZAHANATI YA KISASA VIKAWE

$
0
0
IMG_0282
Mkuu wa Masista Waabuduo Damu ya Kristo, Euprasia Julius akimtambulisha mgeni rasmi na meza kuu kwa wageni waalikwa na wanakijiji wa Vikawe (hawapo pichani) katika hafla ya ufunguzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa Maria De Mathias (MDM) Vikawe, Kibaha.

IMG_0289
Mwenyekiti wa kijiji cha Vikawe, Kibaha, Shabaan Mgini akiwasalimia wageni waalikwa wakati wa utambulisho.
IMG_0301
Sr. Theresia Rogatus akisoma risala katika hafla ya ufunguzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa DMD iliyopo Vikawe, Kibaha.
IMG_0323
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi akizungumza kwenye hafla ya ufunguzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa -DMD kijiji cha Vikawe, Kibaha. Kutoka kushoto ni Mdau wa Zahanati hiyo, Dr. Zuberi Mzige wa Hospitali ya Mwananyamala,
IMG_0335
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi akimpa mkono wa shukrani Mfadhili aliyejitolea kujenga Zahanati hiyo Raia wa Italia, Germano Frioni kwa ujenzi wa Zahanati hiyo itakayohudumia wakazi wa kijiji cha Vikawe, Kibaha.
IMG_0341
Masista Waabuduo Damu ya Kristo wakielekea meza kuu kwa mwendo wa madaha huku wakiwa wamebeba zawadi kwa ajili ya kumkabidhi mgeni rasmi na wafadhili waliojitolea kujenga Zahanati hiyo.
IMG_0348
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi (kulia) akimkabidhi zawadi Mfadhili aliyejitolea kujenga Zahanati hiyo Raia wa Italia, Germano Frioni. Anaye shuhudia tukio hilo ni Baba Paroko wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Kalmeri Bunju...
IMG_0351
Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi akikabidhi zawadi kwa wadau waliombatana na Mfadhili aliyejitolea kujenga Zahanati hiyo Muitalia, Germano Frioni.
IMG_0354
IMG_0194
Mganga Mkuu wa halmashauri ya Mji wa Kibaha, Dr. Happniness Ndosi (wa pili kulia) pamoja na Mfadhili wa ujenzi wa Zahanati ya Da.Ma Africa ya kijiji cha Vikawe, Kibaha, Muitalia, Germano Frioni wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Zahanati hiyo inayosimamiwa na Masista Waabuduo Damu ya Kristo nchini.
IMG_0230
Muonekano wa ndani ya Zahanati ya Da. Ma Africa-DMD iliyop Vikawe, Kibaha mkoa wa Pwani.
IMG_0211
Mganga Mkuu wa halmashauri ya Mji wa Kibaha, Dr. Happniness Ndosi akiangalia chumba cha dawa katika Zahanati hiyo mara baada ya kuzinduliwa.
IMG_0235
Wageni waalikwa wakijadiliana jambo mara baada ya kufungiliwa rasmi Zahanati hiyo nje ya moja ya chumba cha upasuaji mdogo.
IMG_0128
Baba Paroko wa Parokia ya Bikira Maria wa Mlima Kalmeri Bunju akiendesha ibada takatifu ya misa maalum kabla ya ufunguzi rasmi wa Zahanati hiyo.
IMG_9973
IMG_0089
Wanakijiji wa Vikawe wakishiriki ibada maalum wakati wa uzinduzi wa Zahanati ya Da. Ma Africa.
IMG_0126
IMG_0086
IMG_0265
Kwaya ikitoa burudani.
IMG_0017
Wageni waalikwa na wanakijiji wakishiriki kuimba pamoja na kwaya.
IMG_0102
Pichani juu na chini ni baadhi ya wanakijiji na wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi huo.
IMG_0140
Umati wa wageni waalikwa na wanakijiji wa Vikawe.
IMG_0361
Mgeni rasmi Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Kibaha, Dr. Happiness Ndosi katika picha ya pamoja na wadau pamoja na wafadhili waliojenga Zahanati hiyo.
IMG_9898
Masista Waabuduo Damu ya Kristo wakifurahia taswira za picha za mnato kutoka kwenye kamera.
IMG_0224
Jenereta la Zahanati ya Da.Ma Africa linalotumika kutoa umeme katika Zahanati hiyo.
IMG_9881
Muonekano wa nje wa jengo la Zahanati ya Da.Ma Africa kabla ya kuzinduliwa rasmi.
IMG_0247
Wanakijiji wa Vikawe na wageni waalikwa wakiingia kukagua Zahanati hiyo mara baada ya kuzinduliwa.
Na Mwandishi wetu, Kibaha
MGANGA Mkuu wa halmashauri ya Mji Kibaha, Dk. Happniness Ndosi amepongeza shirika la masisita wa Waabuduo Damu ya Kristo kwa kufanikisha ujenzi wa zahanati ya kisasa katika kijiji cha Vikawe wilayani Kibaha mkoani Pwani.
Mganga huyo ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla ya uzinduzi wa zahanati hiyo,pamoja na kuwapongeza amesema serikali itaendelea kushirikiana na mashirika yote kwa lengo la kuwezesha kila kijiji kiwe na zahanati na kila kata kituo na kila wilaya kuwa na hospitali.
Aliwapongeza masista hao kwa kuonesha upendo na huruma kama Biblia inavyomsimulia msamaria mwema ambaye alikuta mtu aliyepigwa na majambazi na kumsaidia.
Aliahidi ushirikiano wa serikali katika kufanikisha usajili wa zahanati hiyo na kuendelea kuisaidia hatua kwa hatua hadi inakuwa kituo mpaka watakapofanikisha safari yao ya kuwa hospitali kubwa ya kisasa.
Mganga huyo pamoja na kutoa ahadi hiyo aliwataka wananchi wa Vikawe kutumia huduma hiyo na kwamba zahanati hiyo itakapohitaji msaada wa gari la kubebea wagonjwa (Ambulance) wataletewa kuchukua mgonjwa na kumfikisha panapohusika.
Zahanati hiyo ya DA.MA Africa imejengwa kwa ufadhili wa wakristo wa Italia chini ya usimamizi wa Muitalia, Germano Frioni.
Akitoa salamu zake Muitalia huyo amesema kwamba anawashukuru wakazi wa Vikawe kwa kumpa nguvu ya kusonga mbele hasa kwa kutambua kwamba yeye na marafiki zake wamefanyakazi usiku na mchana kutafuta fedha kwa ajili ya kusaidia marafiki wa Afrika.
Alisema atajitahidi kufanya kila linalowezekana kuhakikisha changamoto za zahanati hiyo zinafanyiwa kazi.
Aliwaomba wananchi wa Tanzania kuendelea kumuombea yeye na wenzake kama Papa Francis anavyoagiza ili malengo ya safari ya kuwapo duniani yafanikiwe.
Alisema kwamba watoto wake Daniel na Marco (kwa sasa wote ni marehemu) ambao ndio kifupi cha zahanati hiyo DA.MA wamemfanya kujitambua na kusaidia wengine katika kuonesha upendo.
Aidha alisema kwamba ataendelea kukumbuka Vikawe kwani alifika mara ya kwanza mwaka 2005 na kuona hali ilivyokuwa ambapo sasa lipo jengo la zahanati hiyo likiwa limekamilika.
Wazo la ujenzi wa zahanati hiyo , lilitolewa na wananchi wa Vikawe kwa Masisita Waabuduo Damu ya Kristo mwaka 2004 wakati wakiwa katika eneo hilo baada ya kununua ekari 40 kwa ajili ya kilimo mwaka 1994.
Alisema pamoja na maombi hayo na wao wenyewe kutambua kwamba kuna mahitaji makubwa ya huduma ya afya japokuwa kuna zahanati ya serikali, hawakuweza kutekeleza maombi ya wanavijiji hadi mwaka 2011 walipofanikiwa kupata ufadhili kutoka Italia na kuanza ujenzi mwaka 2013.
Katika risala yao walisema kwa ushirikiano kati yao na wafadhili hao wamefanikiwa kuwapo kwa zahanati hiyo yenye mahitaji yote ya msingi kwa mujibu wa taratibu za serikali na kuzidi.
Msoma risala alisema kwamba wataendelea kupanua miundombinu mpaka zahanati hiyo ifikie ngazi ya cha afya na baadae hospitali.
Pamoja na ujenzi wa zahanati hiyo ya kisasa masisita hao wameanzisha shule ya awali kuwaandaa wanafunzi wa darasa la kwanza.
Wamesema kwamba wanaamini kwamba wataendelea kushirikiana na wananchi na wadau wengine wa afya katika kuimarisha huduma za hospitali hiyo.
Zahanati hiyo pamoja na vifaa tiba pia ina raslimali ya visima vya maji ya mvua ujazo zenye ujazo wa lita laki moja na kingine lita 49 elfu, wanatumia umeme wa sola na jenereta .
Walisema kwamba wanachangamoto ya kukosa umeme wa Tanesco, barabara nzuri na nyumba za wafanyakazi.

YOLANDA SHAYO BALOZI WA MKOA WA KILIMANJARO ATEMBELEA VITUO VYA WATOTOTO YATIMA

$
0
0
.
 Yolanda Shayo akisaidia kugawa chakula kwa watoto na viongozi wa vituo hivyo,ambapo alishiriki kwa pamoja nao katika chakula cha mchana.
Mrembo aliebuka kidedea kwenye shindano la kumsaka barozi wa mkoa wa Kilimanjaro 2015,Yolanda Shayo ametembelea vituo vya watoto yatima katika eneo la mamba Malangu moshi vijijini.
 
Shughuli hiyo ilifanyika mapema jana ambapo mrembo huyo alitembelea vituo vinee ambavyo ni Msoroe,Mrieni,Kikoro na kotela kwa kugawa vifaa vya shule kwa watoto na kula nao chakula cha pamoja kilichoandaa kwaajili ya watoto hao.
 
Baadhi ya vitu vilivyotolewa na mrembo huyo ni kalamu,madaftari,rula na sabuni za kufulia na kuogea,Yolanda alipata fulsa ya kuongea na viongozi wa vituo hivyo ambapo alibaini changamoto balimbali zinazokabili vituo hivyo.

Yolanda ambae ni Miss Kilimanjaro Ambassador wa mara ya kwanza ameonesha jitihada zake za kuanza kazi ya urembo kwa kuitumikia  jamii yake ambapo alikuwa ana wito huo tangu akiwa mtoto.

Kwa nafasi aliyoipata mrembo huyo ameaidi kuwa kinara kuutangaza utamaduni wa mkoa wa kilimanjaro na kuvitangaza kitaifa na kimataifa vivutio vya utalii vilivyomo ndani ya mkoa huo.

"mbali ya kuwa mrembo na balozi wa mkoa wa kilimnjaro nitahakikisha natumia fulsa hii kupeleka ujumbe mbalimbali kwa jamii yangu ikiwemo kuwahimiza vijana wenzangu kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura katika uchaguzi mkuu utakaofanyika octoba" aliongea Yolanda

CCM KUMEKUCHA, DK. MAGUFULI KUCHUKUA FOMU NEC KESHO

$
0
0
Today at 2:49 PM
Na Mwandishi Wetu
MGOMBEA mteule wa urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli, kesho Jumanne, Agosti 3, 2015, atatinga Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kuchukua fomu ya kuomba kugombea Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba Mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari, leo jijini Dar es Salaam, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amesema, Msafara wa Dk. Magufuli  kwenda kuchukua fomu hiyo, utaanza saa tano asubuhi ukitokea Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam.



Nape amesema, msafara ambao utaambatana na shamrashamra za aina yake, utapita katika Barabara za Morogoro, Bibi Titi Mohammed na Ohio kabla ya kufika Ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi zilizopo Posta House, karibu na makao Makuu ya Jeshi la Polisi.

Amesema, Dk. Magufuli ambaye ataambatana na Mgombea mwenza wake, Samia Suluhu, mbali na makada, wapenzi na wanachama wa CCM, atasindikizwa na viongozi mbaimbali wakiwemo, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

Dk. Magufuli alichaguliwa na Mkutnao Mku wa CCM, uliofanyika Oktoba 11, 2015, mjini Dodoma, baada ya kuwashinda wagombea wenzake, Dk. Asha-Rose Migiro na Amina Salum Ally.

 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari, kwenye Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam. (Picha na Bashir Nkoromo).

NYALANDU ASHINDA KURA ZA MAONI UBUNGE CCM SINGIDA

$
0
0

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu  na mashabiki wake, wakishangilia baada ya Waziri huyo kutangazwa kuwa mshindi wa kura za maoni ya kugombea ubunge katika jimbo la Singida Kaskazini.

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na mkewe Faraja, wakishangilia na wafuasi wao baada ya Nyalandu, kutangazwa kuwa mshindi wa ubunge katika Jimbo la Singida Kaskazini.

Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, ameibuka na ushindi wa kishindo katika kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuwania ubunge Jimbo la Singida Kaskazini.


Nyalandu, ambaye alikitetea nafasi hiyo aliwashinda wagombea wenzake saba waliojitokeza kupambana naye, ambapo aliongoza kwenye kata zote za jimbo hilo na kuwaacha mbali wapinzani wake.


Mwanasiasa huyo kijana na mwenye ushawishi mkubwa, aliongoza katika Kata za Ikhanoda, Msange, Itaja, Mwasauya, Mrama, Maghojoa, Ilongero, Ngimu na kuzidiwa kwa kura chache kwenye kata moja ya Mughamo.


Matokeo ya mwisho yaliyotolewa na msimamizi wa uchaguzi, yamempa ushindi Nyalandu kwa kupata kura 13,738 huku akifutiwa na Justin Monko aliyepata kura 5,648.


Nyalandu aliwaeleza waandishi wa habari kuwa, anamshukuru Mungu na wanachama wa CCM jimboni humo kwa kumpa ushindi wa kishindo na wenye heshima licha ya kufanyiwa mchezo mchafu na wapinzani wake.


Alisema wapinzani wake walicheza rafu za wazi kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo kuleta makundi ya watu ambao hawakuwepo kwenye orodha ya wapiga kura, kuandaa vijana wa kumzomea kwenye mikutano, lakini mwisho wa siku wananchi wameonyesha bado wana muamini na kumchagua kwa kishindo.


“Nimekuwa kwenye siasa kwa muda sasa…lakini katika uchaguzi huu nimefanyiwa rafu nyingi sana na wapinzani wangu ila nashukuru Mungu wananchi wameonyesha bado wananiamini na imani hiyo inatokana na kazi kubwa niliyoifanya kama mbunge wao. Nitaendelea kuwatumikia kwa juhudi na akili zangu zote na kamwe sitawaangusha,” alisema Nyalandu.

ZAHARA ANENA BAADA YA KUSHINDWA KUPATA KURA ZA KUTOSHA

$
0
0
Baada ya kura kutotosha kumfanya apite katika kura za maoni kugombea Ubunge kwa viti vya Vijana mkoani Tabora, Zahara Muhidin Issa Michuzi (pichani) amepokea matokeo kwa moyo mkunjufu na kumpongeza mshindi Irene Uwoya na kumuahidi ushirikiano katika mambo yote mema ya kuendeleza vijana mkoani humo.
Zahara ambaye sasa ataelekeza nguvu zake katika kusaka digrii ya pili ya uchumi, amesema kwamba anawashukuru wajumbe wa mkutano wa uchaguzi, baba yake, mama walezi, kaka Mkala Fundikira wa Tanzania Bloggers Network (TBN) kanda ya Magharibi na wana TBN wote wa ndani na nje ya nchi akiwemo kaka Jeff Msangi wa Canada na Mubelwa Bandio na DJ Luke wa Marekani, wanahabari wote wa makundi ya Whatsapp chini ya Francis Godwin na walimu wake pamoja  na wananchi wote kwa ujumla kwa kumpa heshima ya kumuunga mkono kwa kujitokeza kujaribu kuomba nafasi hiyo.
Amesema kushindwa kwake hakumaanishi lolote zaidi ya kwamba demokrasia imechukua mkondo wake na aliyehitajika kuendeleza mapambano amepita na yeye hana kinyongo naye na ataendelea kuutumikia mkoa wa Tabora  katika nafasi yake ya mtu ambaye si kiongozi.
Zahara ametoa mwito kwa wagombea wa nafasi zote kwamba kushindwa ni moja ya matokeo katika ushindani wowote hivyo ipo haja ya kujenga utamaduni wa kukubali matokeo bila ya hasira ama kinyongo kwani dunia i duara, na kwamba mlango mmoja ukifungwa kuna mwingine utafunguka.
Amesema hana mpango wa kuhama CCM ambayo anaiamini kuwa ni chama ambacho kitaenzi na kutunza hadhi na mustakabali wa Taifa la Tanzania kuliko chama chochote.
"Kushindwa kwangu kupata kura za kutosha sio mwisho wa dunia. Nina imani kwamba wapiga kura walijua wanachokifanya. Mimi ni nani kuwaoneshea kidole?  Maisha yaendelee kama kawaida na Mola awajaalie wote kwa yote" alisema.

BALOZI LIBERATA MULAMULA ATINGA NDANI YA STUDIO YA KILIMANJARO

$
0
0
 Balozi Liberata Mulamula akiwasili nje ya jengo lenye studio ya Kilimanjaro tayari kuongea LIVE katika kipindi cha Jukwaa langu kinachorushwa kila siku ya Jumatatu kuanzia saa 12 jioni mpaka saa 2 usiku saa za Mashariki za Marekanui. anayemfungulia mlango ni Abdul Malik
 Balozi Liberata Mulamula akiingia ndani ya studio akiwa amesindikizwa Harriet Shangarai (kushoto) ambaye pia ni Mkurugenzi wa studio hiyo, kulia ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme na Abdul Malik
 Balozi Liberata Mulamula akipata maelezo kutoka kwa studio meneja ambaye pia ni mtangazaji na mtayarishaji wa kipindi cha Jukwaa langu, Bwn. Mubelwa Bandio (hayupo pichani) Kushoto ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme akifuatilia maelezo hayo.
 Mhe. Liberata Mulamula akiendelea kusikiliza maelezo kutoka kwa meneja wa studio Mubelwa Bandio ambaye ni mtangazaji na mtayarishaji wa kipindi cha jukwaa lako. Kati ni matangazaji maarufu wa Radio ya Times FM na aliyewahi kutangaza  Radio One Bi. Rose Chitalah ambaye pia anamsaidia Mubelwa Bandio katika utangazaji na kuchangia hoja mbalimbali katika kipindi cha Jukwaa langu.
 Balozi Liberata Mulamula akiendelea kujibu maswali ya watangazaji mahiri Mubelwa Bandio (kulia) na Rose Chitalah (hayupo pichani ) na wasikilizaji waliokua na shahuku ya kumuuliza maswali.
  Balozi Liberata Mulamula akiendelea kujibu maswali ya watangazaji mahiri Bwn. Mubelwa Bandio (hayupo pichani ) na Rose Chitalah (kushoto)
 Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme akisikiliza mahojiano na kunakili baadhi ya vipengele katika mahojiano hayo.
 Kutoka kushoto ni Afisa Ubalozi Swahiba Mdeme, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na mtangazaji mahiri Rose Chitalah wakiwa katika picha ya pamoja.
 Kutoka kushoto ni Dj Luke Joe, Meneja wa studio ya Kilimanjaro,  Mubelwa Bandio, Mhe. Balozi Liberata Mulamula na mtangazaji mahiri Rose Chitalah wakipata picha ya kumbu kumbu na Balozi Liberata Mulamula anayemaliza muda wake kama Balozi wa Tanzania nchini Marejkani na Canada na sasa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Viewing all 4405 articles
Browse latest View live